Hakika Yalionikuta Maishani Ni Mengi sehemu ya 09

Nikajiambia yeye ndiye aliyestahili
adhabu aliyoipata lakini mimi
nilikuwa naonewa tu. Nikaapa
kimoyomoyo kama nitasalimika
sitarudia tena kushirikiana na polisi
wasio waaminifu.
Kwa vile nilikuwa hoi, nikaanguka
chini na kupotewa na fahamu.
Nikiwa sijielewi niliota nainuliwa
na mtu aliyenikuta nimeanguka.
“Mbona umelala hapa?” akaniuliza.
“Nlinguka nilikuwa nakimbia”
nikamjibu.
“Oh pole sana. Ulikuwa unakimbia
nini?”
Nikamueleza ule mkasa
ulionitokea.
“Kwani wewe ulikuwa hujui kama
yule bibi na mwanawe Maimuna ni
majini?”
“Nilikuwa sijui. Kumbe majini
wanaishi na binaadamu?”
“Ndio, wanaishi na binaadamu na
wanafanya biashara kama
binaadamu lakini hawapendi
dhuluma”
SASA ENDLEA
“Lakini mimi sijawadhulumu kitu”
“Nani aliyewadhulumu?”
“Aliyewadhulumu wameshamuua”
“Si alikuwa pamoja na wewe?’
“Hapana. Yule alikuwa mkuu
wangu wa kazi. Kila anachoniambia
mimi nafuatisha”
“Sasa mimi nitakusaidia uweze
kurudi nyumbani kwako kwa
sababu mama yake Maimuna
sielewani naye ingawa trunajuana
sana. Kama atakasirika, wewe
utakuwa umeshasalimika”
“Nitashukuru baba kama
utanisaidia kwa hilo, kwa maana
nimekuwa nikihangaika sana
kwenye huu msitu bila kupata njia
ya kutokea”
“Usiniite baba, mimi si baba yako,
umenielewa?”
“Nimekuelewa. Nakushukuru sana
kwa msaad wako”
“Umekosea tena. Usinishukuru
kabla sijakusaidia. Ngoja nikusaidie
ndipo unishukuru”
“Sawa”
“Haya, amka uende zako. Njia ile
pale”
Hapo hapo nikajiona nazinduka.
Nilipofumbua macho nikajiona
nimelala chini ya mbuyu. Mbuyu
wenyewe ulikuwa ni ule Mbuyu
Kenda, mahali niliposhushwa na
pikipiki wakati nakuja kwenye
eneo lile.
Sasa njia nikawa nimeijua.
Niliangukia mahali pengine
nimezindukia mahali pengine.
Kusema kweli nilishukuru kutokea
mahali hapo. Nikatoa simu na
kumpigia yule mwenye bodaboda.
Simu yake ikawa haipatikani.
Nikapiga polisi lakini kwa uoga.
Nilichohofia ni kuwa simu yangu
isije ikapokelewa na Maimuna.
Baada ya simu kuita kwa sekunde
chache ikapokelewa.
“Kituo kikuu cha polisi hapa,
unahitaji msaada gani?” Sauti
iliyosikika ilikuwa ya kiume.
Nikajua sasa simu ilikuwa imefika
polisi.
Nikajitambulisha na kujieleza huku
nikisisitiza kupata msaada wa
usafiri haraka.
Polisi niliyekuwa nikizungumza
naye alikuwa ni Inspekta Benenza.
Nilipompa yale maelezo alishituka
na kutaharuki, akaniuliza.
“Uko sehemu gani?”
Nikamtajia sehemu niliyokuwa.
“Subiri hapo hapo, polisi watafika
sasa hivi. Kwa muda huu jitahidi
kujilinda mwenyewe”
“Sawa afande”
Nikakata simu. Ubaridi uliokuwa
ukipepea ulinidhihirishia kuwa
ilikuwa ni alfajiri. Nilijifuta
michanga kwenye nguo zangu
kasha nikasogea kwenye kiza ili
nisionekane. Macho yangu
yalikuwa yakiangaza kila upande
nikiwahofia Maimuna na mama
yake kunifuata mahali hapo.
Kulikuwa kimya. Sauti zilizokuwa
zikisikika zilikuwa za vidudu
vilivyokuwa vikipigwa na baridi
kwenye vichaka. Ukimya huo
badala ya kunipa matumaini
ulinisababishia hofu. Ulikuwa
ukimya unaotisha.
Nikajiambia kama Maimuna na
mama yake watatokea itabidi
nikimbie kwa miguu kurudi mjini.
Kutokana na hofu hiyo macho
yangu yalizidi kugeuka kila upande
kuhakikisha kuwa hakukuwa na
chochote kinachokuja.
Nilikuwa nikihesabu dakika kwa
wasiwasi. Nilikuwa nikiona polisi
wenzangu walikuwa wanachelewa
kufika mahali hapo. Kuchelewa
kwao kungeweza kuhatarisha
maisha yangu kwani mahali
nilipokuwa usalama wangu
ulikuwa mdogo sana.
Tangu kuzaliwa kwangu sikuwa
nimewahi kufikwa na mkasa wa
kutisha kama ule. Sikuwahi
kuushuhudia mwili wa mtu
ninayemfahamu ukiwa hauna
kichwa wala sijawahi kushuhudia
kichwa cha mtu ninayemfahamu
kikiwa peke yake.
Pia sijawahi kuona majini. Nilikuwa
nawasikia tu na nilikuwa siamini
habari zao. Kadhalika sijawahi
kuona eneo likibadilika na kuwa
msitu tena msitu wa kutisha kama
ule niliouona…
Mwanga wa taa za gari uliotokea
kwa mbali ulikatiza mawazo
yangu. Nikahisi lilikuwa gari la
polisi linalonifuata mimi. Mwanga
huo ulisogea kwa kasi, nikaweza
kuusikia muungurumo wa gari hilo.
Nikajitokeza barabarani ili waweze
kuniona.
Gari hilo likanipita lakini lilikuwa
gari la polisi. Haraka nikatoa simu
yangu na kupiga kiyuo cha polisi.
Alipokea Inspekta Beneza.
“Mimi Martin…”
Kabla sijamwambia nilichotaka
kumwambia alinikatisha.
“Nimeshatuma gari…”
“Gari la polisi limenipita…”
“Limekupita mahali ulipo…
hawakukuona?”
“Nafikiri hawakuniona,
wamekwenda mbali zaidi”
“Ngoja niwapigie, simama kando
ya barabara. Ukiliona gari hilo
linakuja wapungie mkono”
“Sawa afande”
Nikakata simu.
Nilisogea kabisa kando ya barabara
macho yangu yakiangalia upande
ulioelekea lile gari. Gari lenyewe
lilikuwa limeshafika mbali na
sikuweza kuliona tena.
Ghafla nikasikia sauti za watu
wanaozungumza. Nikageuza
macho haraka kuelekea ule upande
niliosikia sauti. Ulikuwa ni upande
ule wa kuelekea kwenye nyumba
ya Maimuna na mama yake.
Nikawaona watu wawili wanakuja.
Nikawagundua. Walikuwa
Maimuna na yule mwanaume wa
kijini aliyekuwa naye. Nilishituka
sana na sikuwa na pa kukimbilia.
Nikajua sasa ninakufa.
“Lazima atakuwa amefika huku”
Sauti ya Maimuna ikasikika.
“Kama amekuja huku tutamuona”
Sauti ya kiume ikamjibu.
“Wewe ndio umekosea, yule
alikuwa amejificha nyuma ya
mlango”
“Tutampata tu, hana ujanja”
Je nini kitatokea? Usikose
kuendelea na hadithi hii

No comments

Theme images by konradlew. Powered by Blogger.