TAMBUA KIASI CHA MIONZI (SAR ) INAYOTOLEWA NA SIMU YAKO NA MADHARA YAKE


 Tunajuwa ni sawa watu tunakwenda na teknolojia lakini kwa upande mwingne ni muhimu sana kutambua baadhi ya mambo ambayo ni muhimu sanaa kwasababu hivi vifaa vya ki elektroniki tunavyo vitumia vimetengenezwa na makemikali ya ajabu ambayo ni sumu mbaya sana kwa afya ya mwanadamu.


Sote  tumeshawahi kusikia kuhusu mionzi kwenye simu huwa inasababisha saratani mara ... Sasa leo tulicheki hili jambo pia.

Unajuwa kwenye vifaa vya simu huwa vinatengenezwa kwa makemikali mbalimbali kwamfano battery la simu huwa linatengenezwa kwa kuchanganyanya makemikali mbali mbali ambapo battery hiyo inapokuwa kwenye simu inatumika huwa inatoa mionzi ambayo ikizidi huwa inakuwa sio mizuri kwa afya ya mwanadamu. Hivyo basi kwa kuliona hili nchi mbalimbali wakaweka sheria kwamba hivi vifaa vya kielectronic ni lazima vipimwe kiasi cha mionzi inayotolewa kabla ya kuingia sokoni sasa hapa ndo tunakuja kwenye lile neno kwenye title kule juu SAR.

SAR

Hili neno ni kifupi cha neno specific absorption rate... Hiko ni kipimo cha mionzi inayofyonzwa na mwili wa binadamu(RF energy) pale unapotumia vifaa vya ki electronic kama vile simu na compyuta. Kwa mujibu wa sheria za nchi mbali mbali ni lazima vifaa hivi vya kielectronic viwe vimepimwa na kuthibitisha kuwa kiasi cha mionzi inayotolewa Hakina madhara kwa binadamu ila sijajua kwa hapa nyumbani Tanzania kama kuna hii kitu sijui.

Je utajuwaje kiasi cha mionzi inayotolewa na simu yako??


Kila kampuni iliyothibitishwa kutoa cm za mkononi basi ni lazima ihakikishe kuwa simu zake zinapimwa kabla ya kuleta simu zake kwenye soko la watumiaji. Mara nyingi kampuni za simu zilizothibitishwa huonyesha kiasi cha mionzi inayotolewa na simu hizo kwenye simu za watumiaji au kupitia tovuti au website za simu hizo. Sasa basi ili kujua kiasi cha mionzi inayotolewa na simu yako fatilia hapo chini...


Kwa watumiaji wa smartphone basi bonyeza *#07# kwenye simu yako na italeta ditails zote. Kama umebonyeza hiyo code hapo na haijaleta kitu chochote(kama mimi) inakubidi uingie moja kwa moja kwenye website ya aina ya simu unayotumia kisha utaingiza namba ya model ya simu yako ( model namba unaipatia kwenye setting kule kwenye about devic

Pia Matumizi ya simu wakati joto lake lipo juu ni hatari kwa kuwa wakati huo ndio simu inatoa radiation kwa kiasi cha juu.

Pia ni vema kutumia earphones wakati unapoongea na simu kwa muda mrefu kwa hii itakusaidia kupnguza kiasi cha mionzi itakayo ingia katika mwili wako


Kwa mujibu wa shirika moja la kimarekani
FCC wametowa kiasi cha SAR ambacho hakina madhara kwaio simu yako ikiwa na kiwango hicha au chini ya hapo basi simu yako itakuwa nzuri kwa matumizi)


Federal Communications Commission (FCC) in the US has set an SAR level of 1.6 W/Kg forphones and the same measurement is followed in India. This means phone below 1.6W/kg are considered good



Thanks

Subscribe with your email 

Written by Alvin Kimaro 

No comments

Theme images by konradlew. Powered by Blogger.